Hosea 13:1-2

Hasira Ya Bwana Dhidi Ya Israeli


1 aWakati Efraimu alipozungumza, watu walitetemeka,
alikuwa ametukuzwa katika Israeli.
Lakini alikuwa na hatia ya kumwabudu Baali
naye akafa.

2 bSasa wanatenda dhambi zaidi na zaidi;
wanajitengenezea sanamu
kutokana na fedha yao,
vinyago vilivyotengenezwa kwa uhodari,
vyote kazi ya fundi stadi.
Inasemekana kuhusu hawa watu,
“Hutoa dhabihu za binadamu
na kubusu sanamu za ndama.”
Copyright information for SwhKC